Makala

Jinsi ya Kuanzisha Kampuni Binafsi Yenye Dhima Ndogo (Private Limited Company) Tanzania Mwaka 2026
2026-08-06 01:35:34
Wasiliana Nasi Sasa

Jinsi ya Kuanzisha Kampuni Binafsi Yenye Dhima Ndogo (Private Limited Company) Tanzania Mwaka 2026

Kampuni Binafsi Yenye Dhima Ndogo ni Nini?

Kampuni Binafsi Yenye Dhima Ndogo (Private Limited Company - Ltd) ni aina ya kampuni inayotumika zaidi na wawekezaji wa ndani na wa kimataifa nchini Tanzania. Kampuni hii inasimamiwa chini ya Sheria ya Makampuni, Sura ya 212 (Companies Act, Cap 212).

Katika kampuni hii, dhima ya kila mwanahisa inazuiliwa kwenye kiasi cha mtaji wa hisa ambacho hakijalipwa, huku kampuni ikiwa chombo cha kisheria kinachojitegemea tofauti na wanahisa wake.

Sifa Kuu za Kampuni Binafsi Yenye Dhima Ndogo;

  • Idadi ya Wanahisa: Angalau wanahisa 2 na wasiozidi 50.

  • Wakurugenzi: Angalau wakurugenzi 2, ambao wanaweza kuwa raia wa Tanzania au wa kigeni.

  • Uhamishaji wa Hisa: Hisa haziwezi kuuzwa kwa umma, na uhamishaji wake unafuata masharti yaliyoainishwa katika Articles of Association ya kampuni.

Mahitaji ya Kuanzisha Kampuni Binafsi Yenye Dhima Ndogo

Kabla ya kuanza mchakato wa usajili kupitia mfumo wa BRELA Online Registration System (ORS), hakikisha umeandaa taarifa na nyaraka zifuatazo:


Hitaji

Maelezo / Nyaraka Zinazo Hitajika

Wanahisa na Wakurugenzi

Angalau wakurugenzi 2 na wanahisa 2. Raia wa kigeni wanatakiwa kuwa na pasipoti halali, huku Watanzania wakitakiwa kuwa na Namba ya NIDA.

Anwani ya Ofisi ya Kampuni

Anwani halisi ya kampuni nchini Tanzania ikijumuisha Mkoa, Wilaya, Kata, Mtaa, Namba ya Kiwanja au alama ya eneo.

Katibu wa Kampuni (Company Secretary)

Kuteua mtu binafsi au kampuni yenye sifa za kisheria kuwa Katibu wa Kampuni.

Mtaji wa Hisa (Authorized Share Capital)

Taarifa za jumla ya mtaji wa hisa pamoja na mgawanyo wa hisa kwa wanahisa.


Hatua kwa Hatua za Kusajili Kampuni kupitia BRELA ORS

1. Fungua Akaunti BRELA ORS;Tengeneza akaunti na uthibitishe taarifa zako kwenye mfumo wa BRELA Online Registration System (ORS).

2. Omba Jina la Kampuni; Wasilisha majina unayopendelea ili BRELA yafanye uhakiki na kuhifadhi jina litakaloidhinishwa.

3. Jaza Taarifa za Kampuni; Weka taarifa zote muhimu ikiwa ni pamoja na; Taarifa za wakurugenzi,Taarifa za wanahisa, Mgawanyo wa hisa, Shughuli za biashara kulingana na ISIC Business Codes.

4. Pakua Fomu Zinazozalishwa na Mfumo; Baada ya kukamilisha taarifa, mfumo utazalisha: Consolidated Form pamoja na Integrity Form. Pakua fomu hizi kwa ajili ya kusainiwa.

5. Saini na Pakia Nyaraka; Saini, weka tarehe na upakie nyaraka zifuatazo, Consolidated Form, Integrity Form, Memorandum and Articles of Association (MemArts)

6. Lipa Ada za Serikali na Pata Cheti cha Usajili; Lipa ada za serikali kupitia Control Number iliyotolewa na mfumo wa BRELA. Baada ya malipo kuthibitishwa, utapokea Cheti cha Usajili wa Kampuni (Certificate of Incorporation) kwa njia ya kielektroniki.

Wajibu wa Kisheria Baada ya Kusajili Kampuni

Baada ya kampuni kusajiliwa, unatakiwa kuendelea kutekeleza wajibu wa kisheria kama ifuatavyo:

  • Kuwasilisha Taarifa za Mwaka (Annual Returns); Kampuni inapaswa kuwasilisha taarifa zake za mwaka BRELA kila mwaka kwa mujibu wa sheria.

  • Kuwasilisha Marejesho ya Kodi; Kampuni inatakiwa kuwasilisha makadirio ya kodi na marejesho ya mwisho ya kodi kwa Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA).

  • Kuripoti Mabadiliko ya Kampuni; Mabadiliko yoyote yanayohusisha, Wakurugenzi, Anwani ya kampuni, Taarifa nyingine muhimu za kampuni, yanapaswa kuripotiwa BRELA ndani ya siku 14 tangu mabadiliko hayo yafanyike.

City Squares Inawezaje Kukusaidia?

Kuanzisha Kampuni Binafsi Yenye Dhima Ndogo hakupaswi kuwa mchakato wenye ucheleweshaji na urasimu.

Kwa uzoefu wa zaidi ya miaka 20 katika ushauri wa biashara na huduma za usajili wa kampuni nchini Tanzania, City Squares inarahisisha mchakato mzima wa usajili wa kampuni yako.

Tunakusaidia katika: Kuandaa Memorandum and Articles of Association (MemArts) zinazokidhi matakwa ya sheria, Kuwasilisha maombi kupitia BRELA, Kukamilisha taratibu za baada ya usajili wa kampuni, Kutoa ushauri wa kisheria na huduma za ukatibu wa kampuni.

Lengo letu ni kuhakikisha kampuni yako inaanzishwa kwa usahihi huku wewe ukijikita katika kukuza biashara yako.

Wasiliana na City Squares

Wasiliana nasi kupitia Connect with us on WhatsApp, ili kupanga mazungumzo na mmoja wa wataalamu wetu wa uwekezaji.


Au, unaweza kujaza fomu ya mawasiliano kwenye Connect with us here, tovuti yetu au kupanga kikao cha ana kwa ana au mtandaoni kwa ushauri wa kitaalamu.

Viungo vya Huduma Zetu

Rasilimali Muhimu

Machapisho ya Hivi Karibuni

06 Aug
Mwongozo wa Usajili wa Ubia na Biashara ya Mtu Binafsi Tanzania
Mwongozo wa Usajili wa Ubia na Biashara ya Mtu Binafsi Tanzania
06 Aug
Kampuni za Uwekezaji (TIC) Tanzania: Jinsi ya Kupata Cheti cha Vivutio vya Uwekezaji
Kampuni za Uwekezaji (TIC) Tanzania: Jinsi ya Kupata Cheti cha Vivutio vya Uwekezaji
06 Aug
Jinsi ya Kuanzisha Kampuni Binafsi Yenye Dhima Ndogo (Private Limited Company) Tanzania Mwaka 2026
Jinsi ya Kuanzisha Kampuni Binafsi Yenye Dhima Ndogo (Private Limited Company) Tanzania Mwaka 2026
06 Aug
Huduma za Usajili wa Kampuni Tanzania (Hatua Muhimu za Kufuata Mwaka 2026)
Huduma za Usajili wa Kampuni Tanzania (Hatua Muhimu za Kufuata Mwaka 2026)

Uko tayari kuanza mradi wako? Omba huduma yako na anza safari yako nasi!

Mtaalamu wa Kimataifa Mohammed bin Rashid bin Adwan

Mtaalamu wa Kimataifa Mohammed bin Rashid bin Adwan